📖 elimu 🌑haibadili 🌎 dunia 📚 elimu 🌔 hubadili 👬🏾 watu na 👨‍👧‍👧 watu 🌏hubadili DUNIA🗼

1.26M Followers

1.26M Followers
1.26M Followers

UGA WA ELIMU

📕📕KARIBU TUSOME SASA KATIKA MAWANDA MAPANA📕📕 📕Tunarahisisha Usomaji📕Soma Kisasa📕

UHAKIKI WA TAMTHILIYA YA NGUZO MAMA YA PENINA MUHANDO (Hassan Lemunje)

NGUZO MAMA 

MWANDISHI: PENINA MUHANDO
WACHAPISHAJI: DUP
MWAKA: 1982
 NGUZO MAMA ---UHAKIKI WA... - OUTSO Kinondoni. | Facebook
UTANGULIZI
Tamthiliya ya Nguzo
Mama
 iliyoandikwa na Penina Muhando inayasawiri na kuyaelezea matatizo
mbalimbali yanayowakabili na kuwaelemea wanawake wengi wa Tanzania na Afrika
kwa ujumla. Wanawake wengi wamekuwa wakinyanyasika kwa kunyanyaswa na kuteswa
na waume zao. Penina Muhando anathibitisha hayo kwa kutueleza maisha waliyokuwa
wakiishi wanawake wa Patata.

FANI
MUUNDO
Msanii ametumia muundo wa moja kwa moja. Tamthiliya
hii imeanza kuonesha jinsi nguzo mama ilivyolala na harakati za kina mama
kastika kunyanyua nguzo mama. Mchezo umegawanyika katika sehemu nne.
MTINDO
Msanii ametumia mtindo wa dayolojia na masimulizi.
Vilevile ametumia lugha ya kishairi ili kuleta mvuto katika mchezo wake. Pia
msanii ametumia nyimbo na mianzo ya hadithi za fasihi simulizi. (uk 3).
MATUMIZI YA LUGHA
MISEMO/ NAHAU
a)
Utakiona
cha mtema kuni (uk 42).
b)
Watoto
ni taifa kesho (uk 55).
c)
Utakufa
kibudu (uk 22).
d)
Akachanganya
ulimi {uk 57).
e)
Dume
Malaya si dume roho yako kusumbua (uk 40).
  METHALI
i)
La
mgambo likilia lina jambo (uk 45).
ii)
Aso
mwana aeleke jiwe (uk 45).
iii)
Umoja
ni nguvu utengano ni udhaifu (uk 33).
TAMATHALI ZA SEMI
TASHIBIHA
*Anatembea kama kapigwa bumbuazi (uk 9).
* Sikilizeni na sauti kama ndege nyikani (uk 30).
*Wanaswagwa kama mbuzi (uk 44).
*Amevaa kama mkulima wa bara (uk 24).
TASHIHISI
-Hasira zikampanda Bi Nane (uk 8).
SITIARI
-Mbwa mume wako
anayefuata wanawakeovyo.
MBINU NYINGINE ZA KISANAA
TAKRIRI
-Wakajaribu , wakajaribu (uk 5).
-Mwachie! Mwachie! Mwachie! (uk 8).
-Toka! Toka! Toka usirudi tena (uk 8).
-Akaenda, akaenda, akaenda (uk 40).
MDOKEZO
*Wakavuta…….wakavuta……….(uk 35).
*Siku moja ………ngojeni niwaoneshe (uk 49).
*Ee ndiyo malezi ya watoto wetu………(uk 52).
*Hebu tutazame kwanza kwanini hawasogei….(uk 58).
TANAKALI SAUTI
*Lu lu lu lu lu lu lu lu lu! (uk 2 na 18).
*Ai ai ai ai ai ai ai ai ai ai! (uk 2).
MATUMIZI YA KIINGEREZA
-My God  (uk 32,
49, 50).
LUGHA ZA MATUSI
-Shika adabu yako
(uk 39).
-Malaya mkubwa wewe (uk 39).
-Mbwa wee! (uk 39).
-Mbwa mume wako anayefuata wanawake ovyo (uk 39).
WAHUSIKA
  1. Bi Moja
*Mke wa Shabani
*Hakuwa na msimamo katika kusimamisha Nguzo Mama.
*Alikuwa na tama.
*Hafai kuigwa na jamii.
2. Bi Pili
*Mke wa Sudi
*Alinyanyaswa na mume wake.
*Ni mvumilivu katika matatizo.
*Ni mlezi bora wa familia.
*Anafaa kuigwa na jamii.
3. Bi Tatu
*Ni mpenda starehe.
*Hapendi kazi ambazo hazina mshahara.
*Anambembeleza mume wake kwa kuogopa kuachwa.
*Hafai kuigwa na jamii.
4. Bi Nne
*Ni mtu asiyependa maendeleo ya wenzake.
*Ana wivu, mbinafsi, mfitini na ana chuki binafsi.
*Hafai kuigwa na jamii.
5. Bi Tano
*Ni mke wa Maganga.
*Ana hasoira sana.
*Hakumpenda Bi Sita.
6. Bi Sita
*Alikuwa kahaba na alikuwa anatembea na waume za watu.
*Ni mkorofi na hakupenda ushirikiano.
*Hafai kuigwa.
7. Bi Saba
*Alifiwa na mume wake.
*Ni mlezi swa watoto.
*Ni kiumbe duni kwani shemeji zake walimnyang’anya
mali zake zote na hata watoto baada ya mume wake kufa.
8. Bi Nane
*Alipenda ushirikiano na swenzake.
*Alikuwa na elimuya kutosha.
*Alipenda kuelimisha wenzakekatika shughuli za
maendeleo.
*Hakuwa na chuki na mtu.
*Anafaa kuigwa.
9. Chizi
*Nmpenda demokrasia.
*Alipiga vita uoga.
*Ni mfichua maovu yaliyoko katika jamii
*Anaonesha wazi matatizo yanayosababisha
wanawakekushindwa kujikomboa.
*Anafaa kuigwa na jamii.
10. Mwenyekiti
*Ni mtu mwenye uongozi mbaya
*Anapenda kusiliza majungu na fitina.
*Anawachukia wanawake wasomi.
*Hafai kuigwa na jamii
.
MANDHARI
Mandhari ya tamthiliya hii ni ya kubuni. Yanasawiri
maisha ya vijijini na kiasi maisha ya mjini, kwani tunaona mwandishi ameonesha
mandhari ya vilabuni, uwanjani na nyumbani. Mandhari yaliyooneshwa yanaoana
sana nan chi za Kiafrikaa vile Tanzania, kwani unyanyasaji na ugandamizwaji wa
wanawake wa Kitanzania ni sawa kabisa na wale wa Patata.
JINA LA KITABU
Jina la kitabu Nguzo Mama linasadifu yale yaliyomo
ndani ya kitabu hiki. Kitaswira “Nguzo Mama” ni umoja wa wanawake Tanzania
(U.W.T) ambao uliundwa kwa lengo la kuwatetea, kuwalinda na kuwapa haki na
maendeleo wanawake sawa na wanaume. Tamthiliya hii inaonesha harakati za
wanawake wa Patata wakiwemo wakulima, wasomi, waalimu, makahaba na wanaungana
kuimarisha umoja na maendeleo yao. Wanafungua miradi mbalimbali kama vile
kushona, kupika pombe, pamoja na tofauti zilizopo kati yao kama vile uzembe,
majungu, fitina na kutoelewana.
KUFAULU NA KUTOFAULU KWA
MWANDISHI
KUFAULU
Kimaudhui mwandishi Penina Muhando amefaulu kwa kiwango cha juu
katika maudhui yaliyomo ndani ya mchezo huu, kwani amefaulu kutueleza matatizo
yaliyowapata wanawake wengi wa Kiafrika hususani  Tanzania.
Kifani, mwandishi ametumia lugha rahisi inayoeleweka, lugha
ya kishairi inayofurahisha pia na nyimbo zinazoburudisha. Hivyo kufanya mchezo
usichoshe.
KUTOFAULU
Kimaudhui, Penina Muhando ameshindwa kutueleza hatma ya wanawake
wa Patata na jamii nzima baada ya kushindwa kuinua nguzo mama.
Kifani, matumizi ya lugha ya matusi ni udhaifu wa mwandishi,
kwani matusi ni lugha isiyotakiwa katika jamii.
Share:

CLIC THE IMAGE SUBSCRIBE NOW

CLIC THE IMAGE SUBSCRIBE NOW
Bofya Picha Hiyo Hapo Juu Kisha Subscribe Channel Yetu ya Online Class Utapata Offer ya Kutumiwa Vitabu vyaasomo Yote Buree Kupitia Whatsap Yako

FUNDISHWA SASA NA TEACHER HASSAN LEMUNJE KWA NJIA YA MTANDAO KWA GHARAMA NAFUU.

FUNDISHWA SASA NA TEACHER HASSAN LEMUNJE KWA NJIA YA MTANDAO KWA GHARAMA NAFUU.
Popote ulipo bofya hapa uanze kufundishwa na Teacher Hassan Lemunje. Utatumiwa notes, voice notes za maelekezo kwa lugha nyepesi, pamoja na huduma ya solving ya mitihani yote ya Necta pamoja na Mock Regions sambamba na mbinu mbalimbali za kujibu na kufaulu mitihani Yako. Huduma hii ni kwa wanafunzi wa Level zote wenye kutumia WhatsApp. Piga Sasa uweze kuunganishwa (0622548220/076910272).

BLOGS AND GRAPHICS DESIGN; CONTACT US

Search This Blog

About Me

My photo
DAR ES SALAAM, MAPINGA BAGAMOYO, Tanzania
HASSAN AMONI LEMUNJE born in 31 August,1998. He is Professional Teacher as he teach various schools in Tanzania includes Mlali Sec school, Hijra Seminary, Jamhuri Sec school and currently at Baobab Sec school, an author, public speaker, Translator, Interpreter, and editor of various books, dissertations, term papers, research proposals, and articles.��His life purpose: To use my God-given talents to inspire, empower and become a good role model by supporting others to develop their potentials to the fullest and leave the world a better place than I found it & Yupo hapa kwaajili ya kukuletea masuala yote ya kitaaluma Nchini Tanzania. Pia anapatikana FACEBOOK TWETER na INSTAGRAM(@TeacherHassanLemunje) Contact me +255622548220 +255769010272