📖 elimu 🌑haibadili 🌎 dunia 📚 elimu 🌔 hubadili 👬🏾 watu na 👨‍👧‍👧 watu 🌏hubadili DUNIA🗼

1.26M Followers

1.26M Followers
1.26M Followers

UGA WA ELIMU

📕📕KARIBU TUSOME SASA KATIKA MAWANDA MAPANA📕📕 📕Tunarahisisha Usomaji📕Soma Kisasa📕

UHAKIKI WA DIWANI YA WASAKATONGE NA MUHAMED SEIF KHATIBU

Academic : Wasakatonge
JINA LA KITABU; WASAKATONGE
MWANDISHI; MUHAMMED SEIF KHATIB
MCHAPISHAJI; OXFORD UNIVERSITY PRESS
MWAKA; 2003

UTANGULIZI
Wasakatonge ni diwani inayozungumzia hali ngumu ya maisha. Matatizo anayoyataja mshairi ni magumu kutibika mfano wa saratani, hata hivyo wananchi wakiungana na kupambana pamoja jamii mpya yenye misingi ya usawa itapatikana.
Diwani ya Wasakatonge ni miongoni mwa diwani za hivi karibuni zinazotanabaisha matatizo mbalimbali yanayoikumba jamii katika maisha yake ya kila siku. Matatizo hayo yanaonekana kuwa kama saratani isiyo na tiba. Hata hivyo, msanii ana matumaini kwamba, iwapo wananchi wa kawaida wataungana na kuamua kupambana, ni dhahiri kwamba matatizo hayo yatatoweka kabisa. Miongoni mwa matatizo hayo yataoneshwa kwenye kipengele cha maudhui huku yakishadidiwa na fani.
MAUDHUI: ni jumla ya mambo muhimu yanayoelezwa katika kazi ya kifasihi. Maudhui yanajengwa na vipengele vidogovidogo vifuatavyo; dhamira, ujumbe, mgogoro, mtazamo na falsafa.
DHAMIRA: ni jumla ya maana anayovumbua mwandishi aandikapo kazi yake na jumla ya maana anayoipata msomaji pindi anapoisoma kazi fulani ya kifasihi. Kifasihi kuna aina mbili za dhamira yaani dhamira kuu na dhamira ndogondogo. Dhamira kuu ni lile wazo kuu la mwandishi katika kazi, wakati dhamira ndogondogo ni zile dhamira zinazojitokeza ili kuipa nguvu dhamira kuu. Dhamira zilizojitokeza katika diwani hii ni kama ifuatavyo:
UONGOZI MBAYA: ni aina ya uongozi ambao haujali maslahi ya wananchi na taifa kwa ujumla. Ni uongozi unaotumia mabavu na unaojali maslahi binafsi, yaani haufuati misingi ya utawala wa sharia. Katika diwani hii msanii anaonesha kuwa nchi nyingi duniani hasa zile za kiafrika zinakabiliwa na tatizo la uongozi mbaya. Viongozi walio wengi ni madikteta ambao hawataki kuachia madaraka wala kuwapa watawaliwa uhuru wa kuzungumza.
Hali hii tunaopata katika shairi la “MADIKTETA” (uk.21) ambapo msanii anasema kuwa harakati za kusaka uhuru au demokrasia kwa njia ya mtu haijawahi kuzaa matunda yanayotarajiwa. Harakati hizi zimekuwa zikizalisha viongozi “Miungu watu” au marais walio madikteta, kama ilivyokuwa kwa Mabutu Seseko-huko Zaire (kwa sasa DRC), Bokosa-huko Afrika ya Kati na Idd Amini-huko Uganda. Madikteta hawa wamekuwa na kila aina ya uovu ikiwa ni pamoja na kukumbatia ukabila, udini na uvamizi kwa nchi nyingine. Haya tunayapata katika shairi la “SADDAM HUSSEIN” (uk.26:4) anasema;
4.    “Nakuafiki, Saddam, si kwa uvamizi wako,Na ujue kwamba,
                                                  Huo si uasi
                                      Kwa wakubwa mila, 
                                Saddam, yamesha tendeka sana!”
Viongozi wa aina hii huwanyima wananchi wao uhuru wa kusema ikiwa ni pamoja na ule wa kujiamulia mambo yao wenyewe kama katika shairi la “MARUFUKU” namba 45 (uk.36)
                               “Sitakiki uone,
Ingawa una macho,
      Sitaki useme,
Ingawa una mdomo,
                   Sitaki usikie,
Ingawa una masikio,
      Sitaki ufikiri,
Ingawa una akili,
                   Sababu utazinduka,
Utakomboka,
                   Uwe mtu,
Hilo sitaki,
                    Marufuku.”     
Viongzozi wabovu (madikteta) ni wapenda dhuluma na manyanyaso. Huwadhulumu na kuwanyanyasa raia wao na raia wa nchi nyingine kama inavyojidhihirisha katika mashairi ya “KOSA” (uk.3), na “FAHARI LA DUNIA” (uk.45). Katika shairi la “KOSA”, tunaona kuwa unyanyasaji wa wananchi wa kawaida hutokea pale ambapo wanapokuwa wanadai haki zao. Mshairi anasema:
3. “Kosa letu kubwa,
     Kudai haki?
    Yetu miliki?
   Mna hamaki,
       Na huku mnatukashifu!”
Katika shairi la “FAHARI LA DUNIA” (uk.45) tunaambiwa kuwa kuna kiongozi mwenye nguvu (Marekani) ambaye mchana kutwa usiku kuchwa linanyanyasa nchi nyingi bila sababu za msingi. Msanii anasema:
 5.     “Fahari la Dunia,
    Kwa kiburi, linatesa,
       Lajigamba,
      Linatamba,
                Kuwa mwamba,
               Linaoneya.”
 Viongozi wabovu siku zote ni wanyonyaji na hushirikiana na watu wengi wenye nguvu kubeba mirija ya unyonyaji na kuanza kuwanyonya raia wa kawaida. Hali hii hujitokeza sana katika nchi za Dunia ya tatu. Haya yote tunayapata katika mashairi ya “MVUJA JASHO” (uk.12-13), “MIAMBA” (uk.29-30), “MUMIANI” (uk.34) Katika shairi la “MVUJA JASHO” msanii anaonesha kuwa raia wa kawaida wanafanya kazi kubwa na ngumu sana lakini malipo yao hayalingani na jasho wanalolitoa. Katika shairi la “MIAMBA” tunaambiwa kuwa wanyonge hawana chao, jasho lao na wao wenyewe ni chakula cha wakubwa na watawala wao. Ubeti wa 4 wa shairi hili msanii anahoji juu ya suala hili kwa kutumia taswira ya wanyama:
4. “Wanyonge,
     Wamo shidani,
     Digidigi na nyani,
     Wamo makimbizoni,
     Fisi wafurahia,
                    Ni sharia za mbuga?”
Katika shairi la “MUMIANI” linaonesha waziwazi unyonyaji unaofanywa na viongozi au watu wa tabaka la juu dhidi ya tabaka la chini ambao wanaishi vijijini na mijini, waendao hospitalini na wapelekwao mahakamani. Katika ubeti wa 1 tunaambiwa kuwa:-
1.      “Mumiani,
Mijini,
Watembea kwa mato,
Kuzifanya kazi zao,
Kuzinyonya damu zetu,
Hawangoji,
   Tulale.”
Diwani hii inaendelea kuonesha kuwa viongozi wabovu ni wasaliti na wanafiki. Viongozi hawa wanakuwa wepesi kuwaomba wananchi ili kufanikisha jambo fulani. Lakini pindi jambo hilo linapofanikishwa tu viongozi hao huwaweka wananchi pembeni (huwasaliti wananchi). Miongoni mwa mashairi yanayoonesha usaliti na unafiki wa viongozi wa dini na wa kisiasa ni “SIKULIWA SIKUZAMA” (uk.22-23), “WASO DHAMBI” (uk.1), “UASI” (uk.8), “PEPO BILA KIFO” (uk.14), vilevile shairi la “NAHODHA” (uk.41) linaonesha kuwa kuna viongozi wengi wanaoshindwa kazi lakini hawataki kuachilia madaraka. Hata hivyo msanii anaonesha kuwa viongozi wa aina hii wanaweza kuondolewa madarakani iwapo tu wananchi wote wataungana na kuwapiga vita.

Share:

CLIC THE IMAGE SUBSCRIBE NOW

CLIC THE IMAGE SUBSCRIBE NOW
Bofya Picha Hiyo Hapo Juu Kisha Subscribe Channel Yetu ya Online Class Utapata Offer ya Kutumiwa Vitabu vyaasomo Yote Buree Kupitia Whatsap Yako

FUNDISHWA SASA NA TEACHER HASSAN LEMUNJE KWA NJIA YA MTANDAO KWA GHARAMA NAFUU.

FUNDISHWA SASA NA TEACHER HASSAN LEMUNJE KWA NJIA YA MTANDAO KWA GHARAMA NAFUU.
Popote ulipo bofya hapa uanze kufundishwa na Teacher Hassan Lemunje. Utatumiwa notes, voice notes za maelekezo kwa lugha nyepesi, pamoja na huduma ya solving ya mitihani yote ya Necta pamoja na Mock Regions sambamba na mbinu mbalimbali za kujibu na kufaulu mitihani Yako. Huduma hii ni kwa wanafunzi wa Level zote wenye kutumia WhatsApp. Piga Sasa uweze kuunganishwa (0622548220/076910272).

BLOGS AND GRAPHICS DESIGN; CONTACT US

Search This Blog

About Me

My photo
DAR ES SALAAM, MAPINGA BAGAMOYO, Tanzania
HASSAN AMONI LEMUNJE born in 31 August,1998. He is Professional Teacher as he teach various schools in Tanzania includes Mlali Sec school, Hijra Seminary, Jamhuri Sec school and currently at Baobab Sec school, an author, public speaker, Translator, Interpreter, and editor of various books, dissertations, term papers, research proposals, and articles.��His life purpose: To use my God-given talents to inspire, empower and become a good role model by supporting others to develop their potentials to the fullest and leave the world a better place than I found it & Yupo hapa kwaajili ya kukuletea masuala yote ya kitaaluma Nchini Tanzania. Pia anapatikana FACEBOOK TWETER na INSTAGRAM(@TeacherHassanLemunje) Contact me +255622548220 +255769010272