📖 elimu 🌑haibadili 🌎 dunia 📚 elimu 🌔 hubadili 👬🏾 watu na 👨‍👧‍👧 watu 🌏hubadili DUNIA🗼

1.26M Followers

1.26M Followers
1.26M Followers

UGA WA ELIMU

📕📕KARIBU TUSOME SASA KATIKA MAWANDA MAPANA📕📕 📕Tunarahisisha Usomaji📕Soma Kisasa📕

UHAKIKI WA DIWANI YA MALENGA WAPYA BY TAKILUKI (Hassan Lemunje)

HAKIKI WA DIWANI YA MALENGA WAPYA

WAANDISHI: TAKILUKI

WACHAPISHAJI: O.U.P

 MWAKA : 1997

UTANGULIZI
Malenga Wapya | Text Book Centre

MALENGA WAPYA ni diwani yenye mkusanyiko wa mashairi yapatayo thelathini na saba (37) yaliyoandikwa na washairi wapya(malenga wapya). Washairi hawa ni wanafunzi wa Taasisi ya Kiswahili na Lugha za Kigeni huko Zanzibar.

Katika diwani hii ,washairi wamejadili masuala mbalimbali yanayotokea katika jamii. Baadhi yake ni masuala ya kisiasa, kiuchumi, kijamii n.k.Washairi hawa wamejadili masuala ya msingi katika kujenga jamii mpya na kama yatazingatiwa mabadiliko chanya yatatokea kwenye jamii.

MATUMIZI YA LUGHA

Katika ushairi kipengele cha lugha huhisisha taswira, tamathali za semi, methali, nahau,misemo na mkato wa maneno.

Taswira (picha/jazanda) hiki ni kipengele cha lugha ambacho huchora au huwasilisha wazo kwa kutumia picha au taswira mbalimbali,mfano katika shairi la SAMAKI MTUNGONI kuna taswira ya samaki ikiwakilisha watu wa tabaka la chini (watawaliwa), taswira ya mvuvi ni watu wa tabaka la juu (viongozi) na taswira ya mtungo ni sheria,kanuni au taratibu zinazotumiwa kuwabana watu wa tabaka la chini.

  Ø Njiwa  mpenzi shairi la NIPATE WAPI MWINGINE?

  Ø Punda- tabaka linalokandamizwa (shairi la PUNDA)

  Ø Ua – mwanamke/ msichana (shairi la UA)

METHALI

Kuna methali mbalimbali zimetumiwa katika diwani hii; mfano

  Ø Subira yavuta heri (shairi la SIHARAKIE MAISHA)

  Ø Aisifie mvua kaloa mwilini mwake (shairi la SISUMBUKIE KICHAA)

  Ø Fahari – wapiganapo nyasi ndizo huonewa (SOKOMOKO BAHARINI)

MISEMO

  Ø Siharakie maisha (SIHARIKIE MAISHA)

  Ø Sisumbukie kichaa (SISUMBUKIE KICHAA)

  Ø Sokomoko baharini (SOKOMOKO BAHARINI)

TAMATHALI ZA SEMI

TASHIBIHA

  Ø Ubaguzi umezama kama nguzo (shairi la TUNZO)

  Ø Maisha ni kama njia (shairi la MAISHA NI KAMA NJIA)

  Ø Yametolewa na kombe mithili ya gome la mti (shairi la BAHARI)

TASHIHISI

  Ø Samaki wakasirika (shairi la SAMAKI MTUNGONI)

  Ø Njaa imetuvamia (shairi la ADUI)

  Ø Ua limejituliza (shairi la UA)

  Ø Ulimi ninakuasa (shairi la ULIMI)

TASHITITI

  Ø Katika shairi la MWABAJA MWASEMA NINI?

  Ø Nasikia mwatunga,mwatungani washairi

TANAKALI SAUTI

  Ø Parakacha mlio wa majani makvu (shairi la KWA NINI?)

  Ø Kokoriko – shairi la MKULIMA

TAKRIRI

  Ø Kuna takriri kituo cha mfano shairi la KWA NINI?

MKATO WA MANENO



  Ø Kuna maneno yamekatwa ili kuepuka urari wa vina na mizani mfano “anong’ona (shairi la KWA NINI?).

Bofya Hapa Kuendelea
Share:

CLIC THE IMAGE SUBSCRIBE NOW

CLIC THE IMAGE SUBSCRIBE NOW
Bofya Picha Hiyo Hapo Juu Kisha Subscribe Channel Yetu ya Online Class Utapata Offer ya Kutumiwa Vitabu vyaasomo Yote Buree Kupitia Whatsap Yako

FUNDISHWA SASA NA TEACHER HASSAN LEMUNJE KWA NJIA YA MTANDAO KWA GHARAMA NAFUU.

FUNDISHWA SASA NA TEACHER HASSAN LEMUNJE KWA NJIA YA MTANDAO KWA GHARAMA NAFUU.
Popote ulipo bofya hapa uanze kufundishwa na Teacher Hassan Lemunje. Utatumiwa notes, voice notes za maelekezo kwa lugha nyepesi, pamoja na huduma ya solving ya mitihani yote ya Necta pamoja na Mock Regions sambamba na mbinu mbalimbali za kujibu na kufaulu mitihani Yako. Huduma hii ni kwa wanafunzi wa Level zote wenye kutumia WhatsApp. Piga Sasa uweze kuunganishwa (0622548220/076910272).

BLOGS AND GRAPHICS DESIGN; CONTACT US

Search This Blog

About Me

My photo
DAR ES SALAAM, MAPINGA BAGAMOYO, Tanzania
HASSAN AMONI LEMUNJE born in 31 August,1998. He is Professional Teacher as he teach various schools in Tanzania includes Mlali Sec school, Hijra Seminary, Jamhuri Sec school and currently at Baobab Sec school, an author, public speaker, Translator, Interpreter, and editor of various books, dissertations, term papers, research proposals, and articles.��His life purpose: To use my God-given talents to inspire, empower and become a good role model by supporting others to develop their potentials to the fullest and leave the world a better place than I found it & Yupo hapa kwaajili ya kukuletea masuala yote ya kitaaluma Nchini Tanzania. Pia anapatikana FACEBOOK TWETER na INSTAGRAM(@TeacherHassanLemunje) Contact me +255622548220 +255769010272