📖 elimu 🌑haibadili 🌎 dunia 📚 elimu 🌔 hubadili 👬🏾 watu na 👨‍👧‍👧 watu 🌏hubadili DUNIA🗼

1.26M Followers

1.26M Followers
1.26M Followers

UGA WA ELIMU

📕📕KARIBU TUSOME SASA KATIKA MAWANDA MAPANA📕📕 📕Tunarahisisha Usomaji📕Soma Kisasa📕

UHAKIKI WA NGOSWE PENZI KITOVU CHA UZEMBE NA EDWIN SEMZABA

UHAKIKI wa NGOSWE Penzi Kitovu cha Uzembe

UHAKIKI WA TAMTHILIYA YA NGOSWE – PENZI
KITOVU CHA UZEMBE
MTUNZI: EDWINI
SEMZABA
WACHAPISHAJI:THE
GENERAL BOOKSELLERS LTD
CHAPA YA 1-1988
UTANGULIZI

Ngoswe-penzi Kitvu cha Uzembe  inaonyesha namna jamii inapaswa kushiriki
mipango mbalimbali ikiwepo ya kisiasa kiuchumi na kiutamaduni.Mafanikio ya
mipango hiyo inategemea na kujulikana kwa idadi ya watu utayari,uelewa wa watu
hao kuhusu mipango husika
Tamthiliya hii inaonyeshakazi
ya kuhesabu watu ilivyokwama kijijini kwa mzee mitomingi ngengemkeni kutokana
na uzembe wa afisa wa kuhesabu sensa Ngoswe.

FANI
Vipengele vya fani katika kazi
ya fasihi ni muundo ,mtindo,madhari ,wahusika na matumizi ya lugha
MUUNDO
Muundo uliotumika katika tamthiliya
ni wamuundo
wa moja kwa moja ambapo kazi nzima ipo katika sehemu tano ambazo
mwandishi amezipa majina ya kitwasira kulingana na ukubwa wa tatizo
linalozungumziwa ,yaani ameonyesha kuingia kwa Ngoswe kijijini mazingira yanayoashiria
hali ngumu ya maisha(kijito)
Ø
Sehemu
ya pili inaonyesha kazi ya kuhesabu watu imeanza na watu hawana utayari na
uelewa juu ya sensa (vijito)
Ø
Sehemu
ya tatu inaonyesha Ngoswe ameanza kujihusisha na mapenzi na ulevi,ambavyo ni
viashiria vya kuharibu kazi yake (mto)
Ø
Sehemu
ya nne inaonyesha kazi aliyopewa Ngoswe tayari imekosa mwelekeo,Ngoswe amebobea
kwenye mapenzi na ulevi, karatasi zinachomwa moto baada ya kumtorosha Mazoea (jito)
Ø
Sehemu
ya tano inaonyesha serikali ikimuhukumu Ngoswe juu ya takwimu zilizoungua moto
na Ngoswe asingizia kuwa kijijini kuna shida ya kuhesabu kwani nyumba
zimejitenga na watu wenyewe kutoelewa (baharini)
MTINDO
Mtindo uliotumika ni wa kidayalojia
ambapo wahusika wake wanazungumza kwa kujibizana
Pia kuna matumizi ya nafsi zote
tatu na nafsi hizo zimetumika katika sehemu mbalimbali.Mfano sehemu ya tano kwa
matumizi ya nafsi ya kwanza pale Ngoswe anapoulizwa na serikali kuhusu takwimu
akajibu “usemi sinao”
MANDHARI
Kitabu hiki kimejengwa katika
mandhari ya kijijini,hii inadhihirishwa na ukosefu wa huduma muhimu kama vile
shule hospitali na miundo mbinu
Tabia za wahusika pia
zinaonyesha mandhari ya kijijini mfano,ulevi wa pombe za mnazi,watu kutojali
elimu,kun’gan’gania mila zilizopitwa na wakati
MATUMIZI YA LUGHA
Mwandishi ametumia lugha
nyepesi na yenye kueleweka pia mwandishi ametumia tamathali za semi,misemo na mbinu
nyingi za kisanaa.
Tamathali za semi
Hizi ni semi au kauli
zitumiwazo na mwandishi katika kazi ya fasihi ili kuongeza ladha katika kazi
husika
Tashibiha
Ni  tamathali ilinganishayo vitu viwili au zaidi
kwa kutumia viunganishi kama mithili ya ,kama,mfano wa
Mfano,Ngoswe anaposhangaa ardhi
ya kijijini kwa balozi Mitomingi anasema
·
Udongo
mwekundu kama ugoro wa sabiani
·
Tazama
suruali yake kama kengele ya bomani
·
Nikitoka
hapa najitupa kitandani kama gogo
Tafsida
Ni tamathali itumiwayo
kupunguza ukali wa maneno
mfano Mainda anasema labda
anajisaidia(Uk 21)
Takriri
ni tamathali inayorudiarudia
neno ili kuweka mkazo juu ya kile kinachosemwa
Mfano; karibu,karibu(pale
Ngoswe alipokuwa akikaribishwa)
Mdokezo
Ni tamathali ambayo hueleza
jambo kwa kukatakata maelezo
Mfano Mazoea anasema
sijui……sijui……siwezi namwogopa baba (Uk 22)
Tanakali za sauti
Ni tamathali inayoiga mlio wa
vitu
mfano Ngoswe alishindwa
kujizuia akacheka ha ha ha ha
Methali
Ngoswe anamwambia Mazoea
v  “Penye nia pana njia” (uk 22)
Misemo
  v
Hebu
keti tutupe mawe pangoni
  v
Kupeleka
chakula ndio unafanya makambi
Taswira/Jazanda
Taswira mbalimbali zimetumiwa
na mwandishi katika tamthiliya hii. Msanii ametumia taswira ya mtu kwa kuhusisha
na matukio ya wahusika.Mwandishi analinganisha mwanzo wa mchezo ni kijito ni
mto mdogo sana hivyo maelezo ya sehemu hii yanategemewa kuwa madogo sana
  v
Sehemu
inayofuata ya vijito,sehemu ya vijito inaonyesha kuwa masuala                  yanashughulikiwa
na kujadiliwa hapa yanaongeza uzito ingawa sio mazito sana
  v
sehemu
ya mto inaonyesha ukubwa wa shughuli ya
Ngoswe yuko kazini (yuko m toni)tayari yupo ndani ya jukwaa bila shaka maji ya mto
ni mengi (matatizo mengi)na hivyo yeyote atakayeingia mtoni yampasa awe
mwangalifu
  v
sehemu
ya jito inaashiria kuna hatari, kuna matatizo mengi, katika jito kulivika si
kazi rahisi hatimaye tunaonyeshwa Ngoswe amezama baharini ambapo kuzama kwa
Ngoswe ni baada ya makaratasi kuchomwa moto.
WAHUSIKA
Wahusika ni watu walioshiriki
katika mchezo au tamthiliya husika.
Mwandishi amegawa wahusika
katika makundi mawili yaani mhusika mkuu na wahusika wasaidizi
MHUSIKA MKUU
NGOSWE
Ni msomi anayependa kazi ya
kuhesabu watu lakini kutokana na tamaa ya mwili wake anaharibu kazi baada ya
takwimu zote kuchomwa moto na Mitomingi kutokana na kitendo cha kujaribu
kumtorosha mazoea .
WAHUSIKA WADOGO
Mazoea
  v
Msichana
mwenye umri wa miaka 18-20
  v
Ni
mtoto wa balozi (Mitimingi)
  v
Anawakilisha
wanawake wasio na msimamo katika mapenzi
Ngengemkeni mitomingi
  v
Huyu
ni balozi
  v
Baba
yake Mazoea
  v
Anachoma
karatasi za takwimu kutokana na Ngoswe kutaka kumtorosha Mazoea
  v
Ni
mzee aliyeshikilia ukale na anapenda ndoa za mitara
JINA LA KITABU
Ngoswe penzi kitovu cha uzembe
jina hilo la kitabu linasadifu yaliyomo ndani ya kitabu ,kwani msanii kwa kiasi
kikubwa amejaribu kujadili na kuonyesha matatizo yanayoikumba jamii katika
shughuli za kijamii,matatizo hayo ni kama uchawi ulevi uzembe na dhana nyingine
potofu
KUFAULU NA KUTOFAULU KWA
MWANDISHI


Mwandishi katika tamthiliya hii
amefeli kwa kuwa ameonyesha matatizo yaliyomo katika jamii bila kuonyesha mbinu
mbadala ya kuyatatua.

BOFYA HAPA KUENDELEA NA UHAKIKI WA MAUDHUI
Share:

CLIC THE IMAGE SUBSCRIBE NOW

CLIC THE IMAGE SUBSCRIBE NOW
Bofya Picha Hiyo Hapo Juu Kisha Subscribe Channel Yetu ya Online Class Utapata Offer ya Kutumiwa Vitabu vyaasomo Yote Buree Kupitia Whatsap Yako

FUNDISHWA SASA NA TEACHER HASSAN LEMUNJE KWA NJIA YA MTANDAO KWA GHARAMA NAFUU.

FUNDISHWA SASA NA TEACHER HASSAN LEMUNJE KWA NJIA YA MTANDAO KWA GHARAMA NAFUU.
Popote ulipo bofya hapa uanze kufundishwa na Teacher Hassan Lemunje. Utatumiwa notes, voice notes za maelekezo kwa lugha nyepesi, pamoja na huduma ya solving ya mitihani yote ya Necta pamoja na Mock Regions sambamba na mbinu mbalimbali za kujibu na kufaulu mitihani Yako. Huduma hii ni kwa wanafunzi wa Level zote wenye kutumia WhatsApp. Piga Sasa uweze kuunganishwa (0622548220/076910272).

BLOGS AND GRAPHICS DESIGN; CONTACT US

Search This Blog

About Me

My photo
DAR ES SALAAM, MAPINGA BAGAMOYO, Tanzania
HASSAN AMONI LEMUNJE born in 31 August,1998. He is Professional Teacher as he teach various schools in Tanzania includes Mlali Sec school, Hijra Seminary, Jamhuri Sec school and currently at Baobab Sec school, an author, public speaker, Translator, Interpreter, and editor of various books, dissertations, term papers, research proposals, and articles.��His life purpose: To use my God-given talents to inspire, empower and become a good role model by supporting others to develop their potentials to the fullest and leave the world a better place than I found it & Yupo hapa kwaajili ya kukuletea masuala yote ya kitaaluma Nchini Tanzania. Pia anapatikana FACEBOOK TWETER na INSTAGRAM(@TeacherHassanLemunje) Contact me +255622548220 +255769010272