📖 elimu 🌑haibadili 🌎 dunia 📚 elimu 🌔 hubadili 👬🏾 watu na 👨‍👧‍👧 watu 🌏hubadili DUNIA🗼

1.26M Followers

1.26M Followers
1.26M Followers

UGA WA ELIMU

📕📕KARIBU TUSOME SASA KATIKA MAWANDA MAPANA📕📕 📕Tunarahisisha Usomaji📕Soma Kisasa📕

UHAKIKI WA TAMTHILIYA YA ORODHA BY STEVE REYNOLDS (Hassan Lemunje)

Uhakiki wa Tamthiliya ya Orodha ~ Mwalimu Makoba

UHAKIKI WA TAMTHILIYA YA ORODHA
Mtunzi: Steve
REYNOLDS
Mchapishaji : Macmillan
Chapaya
1;2006
UTANGULIZI
ORODHA ni
miongoni mwa tamthiliya ambazo zinaonyesha namna jamii hususani watoto na
vijana wanavyoangamia kutokana na UKIMWI.Vijana wengi wanaangamia kwa sababu ya
ukosefu wa elimu sahihi kuhusu UKIMWI hali hii yaweza kusababisha ongezeko la
waathirika,Binti mdogo furaha kwa kutokujua athari za UKIMWI anajiingiza kwenye
vitendo vya ulevi na uzinzi kama alivyoshauriwa na rafiki yake Marry na
kujikuta akipata UKIMWI mapema hivyo ni vyema asasi kama za dini zihusike
katika kutoa elimu hiyo

FANI
Mwandishi
amewagawa wahusika katika makundi mawili yaani wahusika wakuu na wahusika
wasaidizi
A.   WAHUSIKA WAKUU
·
Mhusika
mkuu katika tamthiliya hii ni Furaha,
·
Msichana
aliehitimu darasa la saba,
·
Furaha
alijihusisha katika mambo ya uzinzi akiwa na umri mdogo
·
Furaha
hakuwa mtiifu kwa wazazi wake kwani licha ya kukatazwa tabia ya utoro wa usiku
na ulevi hakuacha tabia hiyo bali aliendelea mpaka alipopata maambukizi ya VVU
·
Hakuwa
mwaminifu kwa mpenzi wake Salim,alikuwa muongo kwani alimdanganya Salim hana
mwanaume mwingine zaidi yake,
·
Alijihusisha
kimapenzi na watu waliomzidi umri ambao sawa na baba yake mfano bwana Ecko na Padri James
·
Alikuwa
na tama ya pesa na vitu ,alidanganyika kirahisi mfano Marry alimdanganya kuwa
mwema kwa akina bwana Ecko.
·
Si mwaminifu,
·
Muwazi,
·
Mwenye
upendo yuko mstari wa mbele kupambana naVVU/UKIMWI
B.   WAHUSIKA WASAIDIZI
Mama Furaha
·
Ni
mama mzazi wa Furaha
·
Ni
mchapakazi
·
Ni
mpole
·
Ni
mama mwenye upendo
·
Mkweli
·
Ni
muwazi
·
Ana
msimamo
·
Anafaa
kuigwa na jamii kwani ni mama aliyeejishughulisha  katika ulezi wa watoto na familia nzima
Baba Furaha
·
Ni
baba mzazi wa Furaha
·
Ni
mkali
·
Ana
upendo
·
Ana
lugha kali kwa wanae
Marry
·
Ni
msichana
·
Ni
rafiki yake Furaha
·
Ni
Malaya
·
Mlevi
·
Hafai
kuigwa na jamii
Bwana Ecko
·
Ni
mwanaume mtu mzima
·
Ni
mfanya biashara
·
Ni
mlevi
·
Hafai
kuigwa na jamii,sio mwadilifu katika ndoa yake,ni mwathirika wa UKIMWI
Bwana Juma
·
Ni
mwanaume mtu mzima
·
Ni
rafiki yake na bwana Ecko
·
Ni
mzinzi
·
Ni
mtu mwenye tama
·
Ana
lugha chafu hafai
·
Hafai
kuigwa na jamii
Kitunda
·
Ni
kijana wa mtaani
·
Ni
rafiki yake na Furaha
·
Ni
msanii
·
Sio
mwadilifu
·
Sio
muwazi
·
Sio
mkweli
·
Anaweza
kuwa mwathirika wa UKIMWI japokuwa alitumia kondomu baadhi ya siku alizokutana
na Furaha
MTINDO
Mwandishi wa
tamthiliya hii ametumia mitindo mbalimbali katika kazi yake mfano matumizi ya
majibizano (dayaloji)Mtindo huo huruhusu wahusika wake kuzungumza kwa
kujibizana mfano mazungumzo kati ya Furaha na Kitunda
Furaha:kuvuta
nini lako……..(anarudi nyuma)
Kitunda:Mezea
mtoto lazima ujifunze lugha za mitaani
MUUNDO
Mwandishi wa
tamthiliya hii ametumia mtindo wa onyesho ambao sehemu hizo zipo kwenye makundi
matatu ambayo yamejipambanua kutokana na matukio mfano sehemu 1-2 ni mazishi ya
Furaha ,sehemu ya 3-16 ni makuzi ya maisha ya Furaha kwa ujumla ikihusisha
kuugua na kifo chake ,sehemu ya 17-20 ni mwendelezo wa mazishi ya Furaha
ikiwemo mchakato wa kutafuta barua ya furaha (orodha)mchakato unaofanywa a
Bwana Ecko,Padri James na Salim na mwiso wa mazishi ulioamatana na kusomwa
barua ya orodha
MANDHARI
Mwandishi
ametumia mandhari ya kijijini.Hii inawakilisha vijiji mbalimbali hapa Tanzania
na Bara la Afrika kwa ujumla ,mahala ambapo elimu kuhusu UKIMWI haijaeleweka
vema au hakuna kabisa pia huduma za afya kama hospitali hakuna kabisa
MATUMIZI YA LUGHA
Lugha
iliyotumika ni ya kawaida inaeleweka na inazingatia maadili ya kitanzania na
kueleweka vema kwa walengwa na kwa kiasi fulani tamathali za semi na mbinu
nyingine za kisanaa
Misemo/Nahau
Misemo
iliyotumika kwenye tamthiliya hii ni kama ifuatavyo ,
  v
“Shuga
dadi”mwandishi akiwa anamaanisha wanaume wenye umri mkubwa wanaopenda
kutembea na wasichana wadogo umri sawa na binti zao
  v
“mshamba
“mtu ambae hajui mambo ya mjini au mambo ya kileo
  v
“furaha
anavuna mbegu ya kifo aliyoipanda”kuvuna ni msemo                   unaomaanisha kupata
kitu kutokana na matenyo au maandalizi ,msemo huu ni sawa na “utavuna
ulichopanda”
  Ø
MISIMU
Mwandishi
ameweza kutumia lugha ya misimu ili kuweza kumtambulisha muhusika ,misimu
iliyotumika ni ile ya mitaani au ya vijana kutoka kijiweni ,lugha hii tunaweza
kuona ikitumika katika mazungumzo kati ya Kitunda na Furaha mfano
mshikaji,mchizi ,bomba ,poa majani,nitakulinda ,mwanangu ,kuvinjari haya ni
baadhi ya maneno yanayotumika mitaani hususani maneno haya hutumika na vijana
wa kijiweni katika mji
Maana ya
maneno hayo
Mshikaji-rafiki/jamaa
Bomba
mchizi –sawa rafiki/ndugu
Poa-vizuri
/sawa
Ganja,majani-bangi
Nitakilinda-nitakusaidia
Mwanangu-mtu
wa karibu/rafiki yangu
Kuvinjari-kuzunguka/kutalii
TAMATHALI ZA SEMI
Mfano ….yeye
ni kama punda wa kijiji tamathalii hii ilitumiwa kumfananisha Furaha na punda
wa kijiji ambae kila mwaname anampenda ,ilitokana na tabia ya Furaha kuwa
uhusiano wa kimapenzi na wanaume mbalimbali
Pia Kitunda
anafananisha jiji la Dar-es salam sawa na jiji la New york anasema….kisura
sawa na jiji la New york
Pia mwandishi
anapoonyesha namna vipande vya karatasi vilipoanguka baada ya barua ya orodha
kuchanwa na Salim anasema…..vipande vikaanguka kama theluji
  Ø
SITIARI
Tamthiliya hii imetumiwa
na baba Furaha anapofananisha watoto wake ma mbu wanyonyao damu wasioweza
kujitegemea anasema “nyie mbu wadogo”
  Ø
KIJEMBE
Mwandishi
ametumia kejeli kati ya Marry na bwana Juma anasema
Marry:nielezewewe
ni mzee wa kutosha kuwa baba angu
  Ø
TAFSIDA
Pia mwandishi
ametumia tafsida ili kupunguza ukali wa maneno aliyoyatumia
Mfano :Bwana Ecko:Juma hebu mwangalie yule
msichana anavyotingisha kile alichopewa na mama yake
Bwana
Juma:kama ulivyofanya wewe mishikaki yangu midogo
Tamathali
hiyo(tafsida)imetumiwa badala ya kutaja sehemu zake za siri anazozizungumzia
  Ø
TASWIRA
Mwandisha pia
ametumia lugha ya picha(taswira)
Mfano,karibu nitakufa njaa hali nyie mbu wadogo
mnainyonya damu yangu yote,mbu ni taswira inayoonyesha hali ya utegemezi
JINA LA KITABU
Kitabu hiki
kinaitwa ORODHA (The list)neno lenye
maana la mfuatano au mfululizo wa vitabu au mambo.Kitabu hiki kinaonyesha
orodha zifuatazo
Mosi,Orodha
ambayo Furaha alibainisha mambo ambayo yalisababisha kifo chake.mfano;ngono zembe,ukosefu
wa elimu,kukosekana kwa uaminifu,umasikini.
Pili,kuna
orodha ambayo ina mambo ambayo jamii inapazwa kujazingatia ili waepuke UKIMWI
ambayo ni ngono salama,uadilifu,uaminifu,elimu sahihi kuhusuVVU?UKIMWI

BOFYA HAPA KUENDELEA
Share:

CLIC THE IMAGE SUBSCRIBE NOW

CLIC THE IMAGE SUBSCRIBE NOW
Bofya Picha Hiyo Hapo Juu Kisha Subscribe Channel Yetu ya Online Class Utapata Offer ya Kutumiwa Vitabu vyaasomo Yote Buree Kupitia Whatsap Yako

FUNDISHWA SASA NA TEACHER HASSAN LEMUNJE KWA NJIA YA MTANDAO KWA GHARAMA NAFUU.

FUNDISHWA SASA NA TEACHER HASSAN LEMUNJE KWA NJIA YA MTANDAO KWA GHARAMA NAFUU.
Popote ulipo bofya hapa uanze kufundishwa na Teacher Hassan Lemunje. Utatumiwa notes, voice notes za maelekezo kwa lugha nyepesi, pamoja na huduma ya solving ya mitihani yote ya Necta pamoja na Mock Regions sambamba na mbinu mbalimbali za kujibu na kufaulu mitihani Yako. Huduma hii ni kwa wanafunzi wa Level zote wenye kutumia WhatsApp. Piga Sasa uweze kuunganishwa (0622548220/076910272).

BLOGS AND GRAPHICS DESIGN; CONTACT US

Search This Blog

About Me

My photo
DAR ES SALAAM, MAPINGA BAGAMOYO, Tanzania
HASSAN AMONI LEMUNJE born in 31 August,1998. He is Professional Teacher as he teach various schools in Tanzania includes Mlali Sec school, Hijra Seminary, Jamhuri Sec school and currently at Baobab Sec school, an author, public speaker, Translator, Interpreter, and editor of various books, dissertations, term papers, research proposals, and articles.��His life purpose: To use my God-given talents to inspire, empower and become a good role model by supporting others to develop their potentials to the fullest and leave the world a better place than I found it & Yupo hapa kwaajili ya kukuletea masuala yote ya kitaaluma Nchini Tanzania. Pia anapatikana FACEBOOK TWETER na INSTAGRAM(@TeacherHassanLemunje) Contact me +255622548220 +255769010272